Saturday, June 23, 2012

Wakuu habari kutoka Singida hivi punde tu, kwa chanzo cha habari cha kuaminika, zinasema Simbachawene amefumaniwa akiwa na mke wa mtu (mke wa askari mmoja) pale Singida katika Hotel ya Aqua.

Muda huu bado yuko Kituo cha Polisi Mkoa wa Singida akitoa maelezo. Amefumaniwa tangu saa 10 alfajiri. Baada ya kupata tip hiyo, maaskari walikwenda wakazingira hotel hiyo, wakati Simbachawene akitoka yule askari mwenye mke kumbe alikuwa ameficha sime/panga akamkata Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini (Nishati) na Mbunge wa Kibakwe.

Habari zinasema alikuwa yuko njiani kwenda msibani ukweni kwake, Karatu. Hata wakati wa kupiga kura jana jioni hakuwepo bungeni, mintaarafu kuwa anawahi msibani.

Hizo ndizo habari zilizotufikia punde wakuu. Itaendelea kuwa updated kadri iwezekanavyo.
                        Chanzo cha habari http://www.jamiiforums.com

0 comments:

Post a Comment