Wednesday, October 3, 2012


Kuwa na shingo nyeusi ni malalamiko ya kawaida ambapo kuna sababu chache ambazo zinasababisha tatizo hili. Moja ni kutosafisha vizuri shingo yako kwa kuwa na tabia ya kupuuza shingo wakati kusafisha na kuscrub uso. 
Wakati mwingine, hii inasababishwa kwa kuwa na mkusanyiko wa uchafu ambao hufanya ngozi shingoni kuwa nyeusi nakukosa mvuto.

Sababu nyingine ni kwamba shingo ina mikunjo kadhaa ambayo ngozi huwa inahifanyi vumbi na chembe jasho shingoni ambapo baada ya muda husababisha ngozi ya shingoni kuwa na weusi. Kutokana na sababu hizi inakupasa kuwa makini unaposafisha mwili wako hasa sehemu hii ya shingoni.

Ili kuweza kuongoa weusi huu kila siku hakikisha unasafisha ngozi yako ya shingo na kuondoa ngozi iliyokufa kwenye shingo angalau wiki mbili kabla ya kuona matokeo.
  • Tumia maziwa plain kusafisha shingo yako. Maziwa ni cleanser nzuri na vile vile toner nzuri. Baada ya kusafisha, scrub shingo yako na scrub yenye chenga chenga ili kuondoa ngozi iliyokufa. Unaweza kutumia Scrub yoyote kwa ajili ya kuondoa dead skin kwenye shingo yako.
  • Lakini kama hutaki kuwekeza katika moja, unaweza pia kutengeza scrub yako mwenyewe. Unaweza kufanya mchanganyiko wa wa mafuta ya Olive na Sukari kwa kutumia hii scrub shingo yako hii paka kwenye shingo yako pole pole kwa mviringo mpaka sukari iyeyuke yote. Scrub hii itasaidia na hata kuleta tone kwenye ngozi yako.


  • Pia unaweza kufanya mchanganyiko wa walnuts na maziwa ya mtindi na pia ongeza matone kadhaa ya maji ya limau na kisha massage mchanganyoko huu kwenye ngozi yako hatua kwa hatua na taratibu.Kukumbuka kwamba hii ni kidogo abrasive, ukizingatia kuwa walnuts si kama sukari haziwezi kuyeyuka na unatakiwa unapopaka mchanganyiko huu usutumie nguvu maana unaweza ukajiumiza.
 
  • Pia kuna baadhi ya matukio machache na ya kawaida ambayo kwa rangi ya asili ni sehemu ya tatizo. Ufanisi zaidi wa asili ya ngozi unatakiwa huduma ya dawa kwa ajili ya kesi ya rangi ya asili ni kutumia Aloe Vera Gel kwa eneo lenye weusi shingoni mwako. Unaweza kupaka na kuacha Aloe Vera Gel kwenye ngozi yako mara nyingi kama inawezekana.
 

  • Kupaka maji ya limau shingo pia itasaidia kuondoa weusi kwenye shingo kwa kiasi fulani. Lakini kumbuka kufanya hivyo usiku tu, hivyo kwamba huwezi kwenda nje katika jua na mabaki ya maji ya limau kwenye shingo yako. Kama utatoka ukiwa umepaka maji ya limau kwenye shingo wakati wa jua itasababisha ngozi yako kuwa nyeusi.

0 comments:

Post a Comment