Saturday, June 23, 2012

MBUNGE wa Kibaha Mjini, Silvestry Koka (CCM) ametaka kujua mpango wa dharura wa serikali katika kumaliza tatizo la msongamano wa barabara ya kutoka Dar es Salaam kwenda mikoani ambayo inadidimiza uchumi wa nchi.
Akiuliza swali la nyongeza bungeni jana, mbunge huyo alisema tatizo la msongamano katika barabra hiyo ni kubwa na linadidimiza uchumi wa nchi.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Ujenzi, Injinia Gerson Lwenge alisema serikali itazingatia hilo na itahakikisha kunakuwepo na barabara za watembea kwa miguu na zile za magari.
“Watu wanatakiwa kufuata sheria na kuacha kupitisha magari kwenye barabara za watembea kwa miguu, kwani ndicho kitu ambacho kimekuwa kikifanyika, kwa watu wengi wanapoona msongamano umezidi wamekuwa wakikiuka sheria na kupita kwa watembea kwa miguu hiyo sio haki,” alisema Lwenge.

Katika swali la msingi, mbunge huyo alitaka kujua serikali ina mpango gani kabambe wa kupanua barabara ya kutoka Dar es Salaam hadi Kibaha kuwa njia nne au sita, ili kuondoa tatizo hilo la msongamano.
Akijibu swali hilo, Lwenge alisema serikali ina mpango wa kujenga “Express way” kuanzia Dar es Salaam hadi Chalinze kwa kilomita 100 ya njia sita kwa njia tatu kila upande.

0 comments:

Post a Comment