Thursday, March 17, 2016



Simba imebeba wachezaji wake wote kwenda mjini Tanga kuwavaa Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaopigwa Jumamosi. Lakini imewaacha wachezaji hawa wanne.

Kwanza ni Hija Ugando na Mohammed Fakhi ambao ni majeruhi, Hassan Isihaka aliyesimamishwa na Hassan Kessy mwenye kadi tatu za njano.

Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano cha Simba, Haji Manara amethibitisha hilo.

Simba ndiyo vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara wakiwa na pointi 54 wakifuatiwa na Yanga na Azam FC, kila mmoja akiwa na pointi 50, wanapishana idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa.

0 comments:

Post a Comment