Thursday, November 8, 2012

Mheshimiwa Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb.), Waziri wa Uchukuzi, amefuta uteuzi wa Wajube wote wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) kuanzia juzi tarehe 06 Novemba, 2012 na kuteua Wajumbe wengine wanane (8) wanaounda Bodi hiyo. Waziri amechukua uamuzi huo kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo chini ya Kifungu cha 6(2) cha Sheria ya Bandari na Kifungu cha 1(2)(i) cha Jendwali la Kwanza la Sheria ya Bandari ya 2004.

Waliofutiwa ujumbe wa Bodi ni:

1.       Bwana Dunstan G. Mrutu

2.       Eng. George H. Alliy

3.       Mhe. Alh. Mtutura A. Mturur (Mb.)

4.       Bwana Emmanuel Mallya

5.       Bibi Mwantumu J. Malale

6.       Bibi Maria N. Kejo

Kwa bahati mbaya wajumbe wawili wa Bodi hii walipoteza uhai hivi karibuni. Mungu azilaze roho za marehemu hawa mahali pema peponi, Amina.

Walioteulwa kuingia kwenye Bodi hiyo ni:

1.       Dkt. Jabiri Kuwe Bakari

2.       Bwa. John Ulanga

3.       Bi. Caroline Temu

4.       Bwa. Jaffer Machano

5.       Dkt. Hildebrand Shayo

6.       Bw. Saidi Salum Sauko

7.       Eng. Julius Mamiro

8.       Bi. Asha Nassoro

Mabadiliko haya ni sehemu tu ya hatua ambazo Wizara inachukua kurejesha ufanisi katika Mamlaka hiyo ili iweze kuchangia zaidi kwenye pato la Taifa.

Waziri ameiagiza Menejiment ya TPA kuwapa nyaraka zote muhimu Wajumbe wapya wa Bodi ili wajiandae kabla hajakutana nao ndani ya siku kumi kuanzia juzi ili kuingia nao Mkataba wa Ufanisi (Performance Contract).

Ofisi ya Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Uchukuzi
08/11/2012

0 comments:

Post a Comment