Friday, August 31, 2012

Tume ya Taifa ya Uchaguzi  (NEC), imetja majina ya Kata zitakazofanya uchaguzi mdogo wa Madiwani kutokana na wagombea walioshinda katika uchaguzi wa Madiwani uliofanyika Oktoba 31, 2010  baadhi yao kufariki, kupoteza sifa na kujiuzulu.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa tume hiyo, Jullius Mallaba, alisema maandalizi yamekamilika na upigaji kura utafanyika katika vituo vilivyotumika wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.

Aidha, Mallaba alisema watakaohusika katika upigaji kura ni wale walioandikishwa katika daftari la kudumu la wapiga kura ambapo wapiga kura wanatakiwa kwenda kwenye vituo vya kupigia kura wakiwa na kadi zao.

Mallaba alizitaja kata hizo ambazo uchaguzi utafanyika ni:
  • Arusha - Bangata 
  • Arusha - Daraja Mbili
  • Dodoma - Msalato
  • Dodoma - Mpwapwa 
  • Pwani/Bagamoyo - Magomeni
  • Geita - Lwezera 
  • Shinyanga - Bugarama
  • Shinyanga - Mwananza
  • Tanga/Korogwe - Vugiri 
  • Tanga/Korogwe - Tamota 
  • Lindi/Liwale - Makata 
  • Lindi/Nachigwea - Mnero
  • Njombe/Ludewa - Mlangali
  • Njombe/Makete - Luwumbu

  • Ruvuma/Mbinga - Mpepai 
  • Ruvuma/Songea - Mletele
  • Tabora/Sikonge - Ipole
  • Tabora - Miyenze 
  • Tabora - Karitu
  • Mbeya/Mbozi - Mpapa
  • Mwanza/Misungwi - Lubili
  • Kilimanjaro - Kilema Kusini
  • Kilimanjaro - Nanjara
  • Kilimanjaro - Neha 
  • Morogoro/Mvomero - Mtibwa 
  • Morogoro/Ulanga - Mahenge
  • Mtwara/Nanyumbu - Likokona
  • Mtwara/Newala - Kitangiri

0 comments:

Post a Comment