Friday, August 31, 2012

MAHAKAMA ya Rufani imepanga kusikiliza shauri la umri wa msanii wa filamu Elizabeth Michael, maarufu kama Lulu, Septemba 17 mwaka huu mbele ya jopo la majaji watatu wa mahakama hiyo ambao ni Jaji Bernard Luanda, Jaji January Msoffe na Jaji Katherine Oriyo.

Rufaa hiyo ni ile iliyowasilishwa na mawakili wa upande wa mashitaka wakiomba kupitiwa uamuzi wa Mahakama Kuu uliotolewa na Jaji Dkt. Fauz Twaibu ambao alikubali maombi ya Lulu kusikiliza maombi ya utata wa umri wake.

Siku ambayo Mahakama Kuu ilitarajia kuanza kusikiliza maombi ya uchunguzi wa umri wa Lulu, upande wa mashtaka ulidai kuwa umewasilisha Mahakama ya Rufani maombi ya marejeo ya uamuzi huo, jambo ambalo lilifanya Mahakama Kuu iahirishe uchunguzi huo kusubiri uamuzi wa Mahakama ya Rufani.

0 comments:

Post a Comment