Thursday, June 28, 2012


Wauguzi na Madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, wakilisukuma gari la wagonjwa lililombeba mpigania haki zao Dk. Ulimboka wakati akitolewa chumba cha X-ray akipelekwa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI).


Madaktari wakisaidia kumuingiza Dk.Ulimboka katika gari la wagonjwa namba T 151 AVD la Hospitali ya AAR.
Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk. Hellen Kijo Bisimba (katikati), akizungumza na waandishi wa habari Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakati akitoa taarifa ya kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari inayoratibu mgomo wa madaktari nchini, Dk. Stephen Ulimboka, Dar es Salaam jana.
Dk. Cathbert Mchalo wa Taasisi ya Mifupa ya Moi (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumpokea, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania kwa ajili ya kupatiwa matibabu kufuatia majeraha aliyopata kutokana na kipigo.
Ofisa wa Polisi akimzuia mpiga picha wa gazeti la Tanzania Daima, Francis Dande, asimpige picha wakati wakimuondoa askari mwenzao aliyeshambuliwa na madaktari akituhumiwa kukutwa akipiga simu ya kuwataarifu wenzake kuwa Dk. Ulimboka hakufa.

Mmoja wa wana usalama wa (wa pili ushoto), akizozana na madaktari baada ya kumbaini akijifanya ni mwandishi wa habari na kumuamuru kuondoka eneo hilo mara moja.
Mmoja wa madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), wa pili kulia, akizozana na Askari Polisi waliofika hospitalini hapo wakidai wanatafuta redio yao ya mawasiliano iliyopotea wakati wa pilikapilika za kumpokea Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari inayoongoza mgomo wa madaktari nchini, Dk. Stephen Ulimboka, alipoletwa akiwa hoi kutokana na kipigo kutoka kwa watu waliomteka usiku wa kuamkia jana na kumtupa msitu wa Mabwepande.
Madaktari wakiwa wamepigwa butwaa nje ya viwanja vya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kufuatia tukio hilo.

Wauguzi wakiwa nje ya wodi ya Kibasila wakitafakari jambo kufuatia jambo hilo
Wauguzi wakiwa nje ya wodi ya Kibasila wakitafakari jambo kufuatia jambo hilo

0 comments:

Post a Comment