Friday, May 11, 2012


  • Magazeti ya udaku likiwemo hili la Globe yamekuwa yakiandika, tena kama habari kuu katika ukurasa wa mbele kabisa, kwamba Obama ni/alikuwa shoga. Mwanaume mmoja aitwaye Larry Sinclair amekuwa akidai kwamba alikuwa mpenzi wa Obama kwa miaka mingi wakati ule akiwa bado seneta kule jimbo la Illinois; na kwamba walikuwa wanatumia madawa ya kulevya pamoja. Kashfa hizi zilianza zamani wakati Obama bado akiwa mgombea wa uraisi na bado zinaendelea. Larry Sinclair amekuwa akidai kwamba yeye pamoja na mwanaume mwingine shoga aliyekuwa mwimbishaji wa kwaya katika kanisa la zamani la Obama kule Chicago (huyu aliuawa mwaka 2007) waliwahi kuwa na uhusiano wa kishoga na Obama. Hata hivyo alipopewa "polygraph test" ili kuweza kujua kama alikuwa anasema ukweli ama la kuhusu kashfa hizi, alishindwa na matokeo yalionyesha kwamba alikuwa anadanganya.
  • Nyumbani sisi bado tunafikiri kwamba kila kitu kinachoandikwa katika gazeti au kuwekwa mtandaoni ni cha kweli lakini hawa wenzetu wanajua kwamba huu ni udaku na hakuna mtu ambaye anajali. Ndiyo maana Obama aliweza kushinda uraisi pamoja na magazeti haya kuandika udaku wote huu. Siku tutakapoweza kung'amua kwamba mambo mengi yanayosemwa katika magazeti (hasa haya ya udaku yaliyofumuka kila kona ili kuishibisha kiu ya utandawazi) ama si ya kweli au hayajathibitishwa basi tutakuwa tumepiga hatua kubwa. Nimeandika makala ndefu yenye kichwa "Ze Utamu Imetufundisha Nini?" kuhusu jambo hili na makala hiyo itatoka katika gazeti la Kwanza Jamii la Jumanne tarehe 16/6/2009. Nitaiweka hapa baadaye kidogo.
CHANZO CHA HABARI: http://matondo.blogspot.com/2009/06/magazeti-ya-udaku-obama-ni-shoga.html

0 comments:

Post a Comment