Friday, July 22, 2016

Msanii maarufu wa VICHEKESHO (Komedi) Ndugu. Ismail Issa Makombe a.k.a KUNDAMBANDA, amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo.

Kundambanda alikuwa mgombea ubunge wa CUF na UKAWA kwenye jimbo la Masasi - Mtwara katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi Disemba 2015 baada ya ule wa Oktoba kutofanyika kutokana na kifo cha aliyekuwa mgombea wa awali wa UKAWA, Mhe. Emmanuel Makaidi (NLD). Katika uchaguzi huo wa Disemba 2015 Kundambanda alipata kura 14,069 dhidi ya kura 16,597 za (mshindi) Rashid Chua Chua kutoka CCM. Taratibu za mazishi zinafanyikia nyumbani kwao Masasi.  Inna lillah wainailayna rajiun. RIP Kundambanda.

0 comments:

Post a Comment