Tuesday, September 11, 2012


Sakata la uhamisho wa Mbuyu Twite na Kelvin Yondani waliosajiliwa na klabu ya Yanga na kuwekewa pingamizi na timu ya Simba limefikia mwisho

Hatimaye leo hii sakata la uhamisho wa Mbuyu Twite na Kelvin Yondani waliosajiliwa na klabu ya Yanga na kuwekewa pingamizi na timu ya Simba limefikia mwisho baada ya wachezaji hao kuidhinishwa na kamati ya sheria, maadili na hadhi za wachezaji ya shirikisho la soka TFF, chini mwenyekiti mwanasheria Alex Mgongolwa, kuichezea klabu bingwa ya Afrika mashariki na kati Dar Young Africans.

Kwa taarifa za uhakika nilizozipata kutoka ndani ya shirikisho la soka nchini ni kwamba wakati kamati ya maadili na sheria ilipokaa mkutano wa kujadili mapingamizi ya wachezaji hao ilishindikana kabisa kwa wajumbe wa kamati kufikia makubaliano juu ya hukumu ya mapingamizi hayo hasa la Kelvin Yondan na hapo ndipo ikamuuriwa kwamba zipigwe kura miongoni mwa wajumbe kuamua ni wapi mchezaji huyo akacheze msimu kati ya Yanga au Simba ambazo zote zina mkataba naye. Wajumbe wakapiga kura na hatimaye kura nyingi zikachague aidhinishwe ajiunge na Yanga.

Kwa upande wa suala la mchezaji Mbuyu Twitte liliamuariwa kwa Yanga iwalipe Simba kiasi cha $32,000 ambazo Simba walimlipa Mbuyu Twitte ajiunge nayo kabla ya Yanga kuwazidi nguvu mahasimu wao na kumtwaa mchezaji huyo huku akiwa tayari kashasaini mkataba na Simba, malipo haya yafanyike ndani ya siku 21 na baada ya hapo Twitte atakuwa huru kukipiga jangwani.
Chanzo cha habari  www.shaffihdauda.com

0 comments:

Post a Comment