Wednesday, July 4, 2012

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma, Celina Kombani, wakati akijibu hoja za wabunge jana, alisema katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kuna watumishi wengi na hivyo Serikali itafanya tathimini ya kazi ya kila mtumishi ili kufahamu kama wote wanahitajika au la.

Alisema baada ya kutathimini kazi za watendaji wote, wataangalia sifa zao kama zinawaruhusu kuendelea kufanya kazi katika hospitali hiyo na kama haziwaruhusu, watahamishwa.

0 comments:

Post a Comment