
Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael, 'Lulu'.
Vielelezo
 vilivyowasilishwa mahakamani, ni pamoja na CD iliyorekodi mahojiano 
kati ya mtangazaji wa Clouds TV, Zamaradi Mketema, maelezo ya kuomba 
hati ya kusafiria na leseni ya udereva.
Pia 
umewasilisha mahakamani hapo maelezo ya polisi pamoja na maombi ya hati 
ya kusafiria ambapo mshtakiwa ameeleza kwamba ana umri zaidi ya miaka 
18.
Kesi hiyo itasikilizwa Juni 25, mwaka huu, mbele ya Jaji Dk. Faiz Twaib mahakamani hapo.
Juni 13,
 mwaka huu, mawakili wa utetezi, Peter Kiabatala, Fuljensi Massawe na 
Kennedy Fungamtama, waliwasilisha vielelezo kwa njia ya maandishi 
kupitia kiapo.
Katika 
ushahidi uliowasilishwa, baba mzazi wa Lulu, Michael Kimemeta, ameapa 
kwamba, binti yake hadi anatuhumiwa kufanya mauaji, umri wake ni miaka 
17.
Kalugila,
 ambaye ni mama mzazi wa Lulu naye pia anadai kuwa alijifungua mtoto 
huyo miaka 17 iliyopita katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), 
jijini Dar es Salaam.
Upande 
wa Jamhuri unaoongozwa na Wakili wa Serikali, Shadrack Kimario, utajibu 
ushahidi huo Juni 20, na maombi hayo yatasikilizwa Juni 25, mwaka huu.
Lulu 
anakabiliwa na shtaka la mauaji dhidi ya msanii mwenzake, Kanumba Aprili
 7, mwaka huu, katika eneo la Sinza Vatican, jijini Dar es Salaam.
                                           
     CHANZO:
     NIPASHE
    
0 comments:
Post a Comment